1985 - 2008


KARIBU KWENYE SHULE YA UMISHENI
KWA LUGHA YA KISWAHILI

na Mch. Paul Sungro Lee

Karibu Kwenye Shule Ya Umisheni Katika Lugha Ya Kiswahili

Orodha Ya Masomo Kwa Lugha Ya Kiswahili Bila Malipo

Maswali Yaulizwayo Mara Kwa Mara
Kijitabu cha maelekezo kwa wanafunzi, viongozi wa kozi, na wachungaji

In English

 

Karibu kwenye tovuti ya Kiswahili ya Shule ya Umisheni

Kasisi Silas Yego, Makamu wa Askofu wa Africa Inland Church alisema, “Hitaji la Afrika leo ni kupata viongozi wasomi”. Naye Dk. Tite Tienou, Kasisi Kiongozi katika taasisi ya Trinity Evangelical Divinity School aliwahi kusema, “Mbinu za sasa za ufundishaji hazina uwezo wa kukabiliana na hitaji la uongozi katika kanisa la Afrika leo. Afrika inahitaji walimu zaidi”. Shuhuda hizi ni moja tu ya mambo yaliyotusukuma kutafsiri mafunzo haya kwa lugha ya Kiswahili.

Tafsiri hii ya Kiswahili ilifanywa na kikundi cha watumishi waaminifu wa injili nchini Kenya kwa lengo moja la msingi; kuwafundisha washuhudiaji na waanzilishi wa makanisa hapa Afrika katika siku hizi za mwisho. Katika shughuli zangu za kikristo kwenye eneo la kuwaelimisha wahudumu, nilikuwa na ndoto ya kupata muhtasari wenye mafunzo yote muhimu yanayohitajika ili kumwandaa mhubiri kwa ajili ya huduma. Baada ya kupata ujuzi fulani kuhusu namna ya kuwaelimisha wahudumu na kazi ya kuanzisha makanisa katika eneo la Afrika Mashariki kwa miaka kadhaa, nilianza kuelewa kwamba panahitajika kiwango kikubwa zaidi cha juhudi za kuwaandaa wahubiri kwa ajili ya Afrika; mawazo ambayo hayakutofautiana na yale ya viongozi wengine wa kikristo niliowataja hapo juu. Miaka kadhaa iliyopita, Mungu aliniongoza kugundua mpango wa masomo kama ulivyoandikwa na Dk. Les Norman wa DCI Trust huko Uingereza.

Mpango huu wa masomo tuliupokea na kuufanya sehemu ya mkakati wetu wa mafunzo hapa Afrika Mashariki, na umetusaidia kuyafanya makanisa yaliyokuwapo kuanzisha makanisa mengine kwa kuwapa mafunzo viongozi muhimu katika makanisa yao. Ni wazi kwamba huu mkakati wa Shule ya Umisheni umekuwa ni uti wa mgongo wa huduma yetu ya kuanzisha makanisa tangu mwaka 2000. Mimi na wenzangu wengi tumekubali kwamba hii ilikuwa ni kazi ya Mungu kwa jinsi tulivyoona mkakati huu ukichangia kuanzishwa kwa makanisa mapya yapatayo 150 katika kipindi kifupi tu cha miaka mitatu.

Ndipo baadaye tukabaini kwamba iwapo masomo haya yatatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili, kutakuwa na ongezeko la viongozi wa kanisa wasomi, na waanzilishi wa makanisa wanaofahamu vizuri Kiswahili. Baada ya tafsiri hiyo kukamilika, na kama ilivyotarajiwa, kulikuwako na ongezeko la makanisa mapya katika maeneo ya umisheni wetu. Tunaweza kukushuhudia uweza ya mafunzo haya; unatenda kazi kwelikweli katika huduma yetu!

Ni matumaini yetu kwamba utafurahia mafunzo haya kwa lugha ya Kiswahili. Tafadhali yapitie, na iwapo utahitaji taarifa zaidi baada ya kutembelea tovuti yetu, basi usisite kuwasiliana nasi kwa anwani ifuatayo: eaptc@eaptc.org Tutafurahi kukujibu kwa haraka iwezekanavyo.

Kwa mara nyingine napenda kumshukuru kwa moyo wa dhati Dk. Les Norman kwa kuandaa masomo haya. Namshukuru pia kwa kututia moyo wakati tulipokuwa tukifanya kazi ya kutafsiri. Shukrani nyingi zaidi namtolea Bwana Yesu aliyeniita kwenye huduma hii ya ajabu, na kazi ya maana – kuwatumikia watumwa wake!

Karibu Kwenye Shule Ya Umisheni Katika Lugha Ya Kiswahili

Orodha Ya Masomo Kwa Lugha Ya Kiswahili Bila Malipo

Maswali Yaulizwayo Mara Kwa Mara
Kijitabu cha maelekezo kwa wanafunzi, viongozi wa kozi, na wachungaji


With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
for this revision and translation from the original English
mboeradsk @ yahoo.com

 


 1985 - 2007

 
www.dci.org.uk